Friday, September 6, 2013

MAJANGA MENGINE,MWANAMKE AKAMATWA AKISAFIRISHA

Ripoti ya itv.co.tz imeamplfy kwamba mwanamke mmoja raia wa Nigeria amekamatwa na maofisa usalama wa mamlaka ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar-es-salaam akiwa na kete 99 za dawa za kulevya alizokuwa amezihifadhi kwenye chupa ya mafuta ya kupaka na nyingine kwenye kopo la poda za watoto, akijianda kusafiri nazo hadi Rome Italia kupitia ufaransa.
Meneja mkuu wa usalama wa uwanja wa ndege Clemence Jungu amesema kukakamtwa kwa dawa hizo kunafuatia uwanja huo kufungwa mashine za kisasa za kukagulia mizigo ikiwemo dawa za kulevya.
 Kwenye sentensi nyingine, raia mmoja wa Urusi aitwae Romani Demichenco akitokea Berlin Ujerumani kupitia Doha Qatar amekamatwa kwenye uwanja wa ndege Dar es salaam akiwa na vivimiminika vinavyoweza kusababisha milipuko ambapo tayari amefikishwa Mahakamani.IMG_1601

No comments:

Post a Comment